Nabii Eliya

Nabii Eliya

Eliya katika Shirika

Hali ya maisha waliyoishi Wakarmeli wa kwanza ilikuwa ni ya kieliya kiasi kwamba walijisikia kuwa katika hali ya kuwasiliana naye moja kwa moja. Hawakuwa Wakarmeli tu waliokuwa wakivutwa na nabii Eliya bali hata mahujaji wengine wengi wa kipindi kile ambao walikuwa wakiitembelea Nchi Takatifu, walikuwa wakiguswa na maisha yake. Wengi wao waliokuwa wakienda kuhiji Nchi Takatifu walikuwa wakifika pia mlima Karmeli sehemu ambayo Eliya aliishi maisha ya kieremiti. Wakarmeli waliishi mlima Karmeli karibu na chemchemi ya Eliya wakitamani kuwa kama yeye. Walimchagua Eliya “mtu wa jangwa” kuwa kama baba yao na kiongozi wao wa kiroho.Eliya alikuwa ni mtu wa sala na aliishi katika uwepo wa Mungu akimtumikia kwa uaminifu mkubwa. Hata pale wana wa Israeli walipokengeuka, yeye alisimama imara akiitetea imani halisi ya Israeli, imani kwa Mungu mmoja. Kwa maisha yake Eliya anamfundisha kila mmoja wetu jinsi ya kuishi kwa vitendo upendo na imani kwa Mungu. Alipochagua kuishi maisha ya kipweke, ni wazi alikuwa akimfundisha kila mtu njia sahihi ya kuzitawala tamaa za kimwili kwa ajili ya kuwa na moyo safi. Eliya aliishi maisha ya kifukara, maisha ya kijangwa, maisha ya kipweke kwa utakatifu za wazi ulioonekana kwa watu wote (Soma YsB 48:1-11). Kutokana na maisha yake ya kimonaki, anaheshimiwa sana na mababa wengi wa kimonaki ambao wanamwona kuwa yeye ndiye “mwanzilishi” wa maisha hayo. Kwa upande wetu Wakarmeli tunamheshimu kama baba yetu wa kiroho na anatajwa katika vitabu vya kiliturujia vya Shirika.

 Utume wake

Kazi yake ukubwa ilikuwa kuwarudisha kwa Mungu wa ukweli waabudu miungu. Biblia haitaji jina la baba yake wala la mama yake. Ni mfano wa Melkisedeck.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Zingatia: Mwanachama wa blogu hii tu ndiye anayeweza kuchapisha maoni.

Home

Kundi la Wakarmeli Watanzania wa kwanza lililofungua misheni 2009 Bikira Maria na Nabii Eliya katika Karmeli