“Propositum” ya Wakarmeli wa Kwanza
(Propositum maana yake mapendekezo).
1. Wakarmeli wanamwendea Mt. Albert
Wakarmeli walioishi mlima Karmeli walimwendea Mt. Albert –aliyekuwa
Patriarka wa Yerusalemu wakimwomba awapatie Mwongozo wa maisha. Yeye
aliwaambia wamempelekee mapendekezo ya jinsi wanavyotaka kuishi.
Mapendekezo hayo ndiyo yanayoitwa “Propositum”.
2. Lengo- Mambo ya msingi katika Kanuni
Kanuni inasema kwamba ni suala la msingi kwa
mkarmeli “kuishi maisha ya utii kwa Yesu Kristo -wenye moyo
safi na katikadhamiri nzuri, kama ulazima wa
kumwitikia Mwalimu” (namba 2.). Haisemi utii kwa papa au askofu au padre
bali kwa Yesu Kristo. Hiki ni kitu cha kipekee kabisa na cha tofauti.
Kuishi maisha ya utii kwa Yesu Kristo, kunawafanya wakarmeli wajifunge
wao wenyewe hasa katika mambo yafuatayo:
kuendeleza tafakari ya maisha yao, katika majadiliano ya wazi na Mungu
kuishi upendo kamili
kutafakari usiku na mchana Neno la Bwana
kusali pamoja au peke yake mara kadhaa kwa siku
kushiriki adhimisho la Ekaristi kila siku
kufanya kazi za mikono, kama Paulo Mtume alivyofanya
kujisafisha/kujitakasa kwa kila namna dhidi ya uovu
Kuishi umaskini kwa kuweka pamoja vitu vinavyopatikana
kuishi upendo kamili
kutafakari usiku na mchana Neno la Bwana
kusali pamoja au peke yake mara kadhaa kwa siku
kushiriki adhimisho la Ekaristi kila siku
kufanya kazi za mikono, kama Paulo Mtume alivyofanya
kujisafisha/kujitakasa kwa kila namna dhidi ya uovu
Kuishi umaskini kwa kuweka pamoja vitu vinavyopatikana
Kulipendo Kanisa na watu wote
Kukubali matakwa yao yaendane na yale ya Mungu,
kutafuta mapenzi ya Mungu daima katika imani, kwa kupitia mazungumzo
na kupitia utambuzi (discernmen)wa maisha.
Kuwa na maisha yenye utaratibu
Toka mwanzo walikuwa na nadhiri ya kutorudi nyumbani kwao.
Huduma kwa Kristo – kuishi katika kumfuasa Yesu Kristo, “In Obsequio Iesu Christi”. Katika Propositum, anatajwa mtu aliyekuwa kama kiongozi wao, “B”.
Hivyo “Kanuni ya Maisha”, aliyowapatia Mt. Albert, ilitokana na Propositum yao.
3. Norma di Vita, Kanuni ya maisha
Maisha yao yalikuwa ya kimonaki lakini yakiwa na chembechembe za kijumuiya.
Yesu aliwekwa katikati ya maisha yao –kwa neno “obsequio”. Kumtegemea
Yesu kwa kila kitu: Sura-7 na 18. Kristo kama nguvu Sura 10. Kutenda
kadiri ya Nafsi ya Yesu 14. Matunda ya mfufuka Sura ya 9-10. Yote hayo
yanafanyika katika ufunguo wa kitovu cha maisha ya Utatu Mtakatifu Sura
8, 14,15.
Kanuni ya Karmeli kwa kiswahili
1. Albert kwa neema ya Mungu, aliyetwa
Patriarka wa Kanisa la Yerusalemu kwa wapendwa wana katika
Kristo, B. na kwa waeremiti wengine walioko chini ya utii wake, wakaao
kwenye chemchemi katika mlima Karmeli: salamu katika Bwana nabaraka
za Roho Mtakatifu.
2. Mara nyingi na kwa njia
nyingi mababa watakatifu waliweka jinsi kila mmoja katika shirika
lolote au njia yoyote ya maisha ya kitawa aliyochagua
anavyotakiwa kuishi katika utii kwa Yesu Kristo na kumtumikia kwa
uaminifu kwa moyo safi na dhamiri njema.
3. Hata hivyo kwa kuwa mnahitaji kutoka kwetu kwa mujibu wa madhumuni yenu sisi tunawakabidhi ninyi kanuni ya maishaambayo mnatakiwa muifuate katika siku zijazo.
4. Hiki katika nafasi
ya kwanza tunakianzisha kwamba muwe na mkuu miongoni mwenu ambaye
atachaguliwa katika ofisi hii kwa ridhaa moja ya yote au ya sehemu
kubwa na yenye matashi mazuri, ambaye kila mmoja wenu amwahidi utii na
apouahadiajifunze kuutekeleza kwa ukweli wa matendo pamoja na usafi wa
moyo na kujikatalia kumiliki vitu.
5. Mnaweza tena kuanzisha makazi kwenye ueremiti au mahali
mtakapopewa pakufaa na nafuu kwa ajili ya heshima ya shirika lenu kama
ambavyo itakaonekana inafaa kwa mkuu na ndugu.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni
Zingatia: Mwanachama wa blogu hii tu ndiye anayeweza kuchapisha maoni.