Karama ya shirika
Karama ya shirika ni "kuishi maisha ya utii kwa Yesu Kristo". Karama hii imeundwa na mambo makuu matatu:
Maana na matumizi ya neno «karama»
Neno «karama» ni tafsiri ya neno la kigiriki (kiyunani) - "karisma -χἀρισμα "» ambalo nalo limetokana na jina «χἀρις <; - "karis"» yaani, «neema». Ambapo karama (karisma) ina maana ya «zawadi ya kimungu» kilicho kielelezo cha neema ya Mungu anayozawadiwa mwanadamu. Daima neema ni zawadi kutoka kwa Mungu, si kipawa cha asili hata kama hakuna kipawa cha asili kisichokuwa zawadi kutoka kwa Mungu. Lakini hapa tunaongelea neema maalum. Mtume Paulo ndiye aliyelitumia mara nyingi neno karama katika barua zake. Anatumia neno karama kama ipawa au uwezo.
Kwa mfano, anamwandikia Timotheo akimwambia hivi: "Usiache kuitumia karama ile iliyomo ndani yako, uliyopewa kwa unabii na kwa kuwekewa mikono ya wazee" (Tim 4:14), na anaendelea kumwambia, "Kwa sababu hiyo nakukumbusha,
uichochee karama ya Mungu, iliyo ndani yako kwa kuwekewa mikono yangu" (2Tim 1:6).
Anachosema Mtume Paulo ni kuwa: kuishi kwa kiasi, uwezo wa kuongoza waamini na kuwafundisha maadili ya kimungu, kwa ujumla ni zawadi (karama) ya Mungu mwenyewe. Lakini karama hiyo inapatiwa nguvu ya kimamlaka kwa ajili ya kutimiza wajibu wake kwa kuwekewa mikono na wazee na Paulo.
Vile vile Mtume Paulo anawaambia Wakristo wa Rumi: «Kwa maana ninatamani sana kuwaona, nipate kuwapa karama za rohoni, ili mfanywe imara» (Rum 1:11). Ukiendelea kusoma Waraka huo huo kwa Warumi, utakuta Mtume Paulo anaeleza hivi: «Lakini karama He haikuwa kama Hie kosa; kwa maana ikiwa kwa kukosa kwake yule mmoja wengi walikufa, zaidi sana neema ya Mungu, na kipawa kilicho katika neema yake mwanadamu mmoja Yesu Kristo kimezidi kwa ajili ya wale
Wengi» (Rum 5:15).
Na anaitaja tena katika Rum 5:16b akisema: "bali karama ya neema ilikuja kwa ajili ya makosa mengi, ikaleta kuhesabiwa haki"
Kumbe basi Karama ni zawadi kutoka kwa Mungu kwa kanisa kwa ajili ya ulimwengu. Karama ya kila familia ya kitawa ni njia maalum ambayo wanashirika wake wanaitwa kumfuata Kristo kwa mfumo huo wa maisha.
- Maisha ya tafakari
- Maisha ya kindugu na
- Maisha ya huduma
Maana na matumizi ya neno «karama»
Neno «karama» ni tafsiri ya neno la kigiriki (kiyunani) - "karisma -χἀρισμα "» ambalo nalo limetokana na jina «χἀρις <; - "karis"» yaani, «neema». Ambapo karama (karisma) ina maana ya «zawadi ya kimungu» kilicho kielelezo cha neema ya Mungu anayozawadiwa mwanadamu. Daima neema ni zawadi kutoka kwa Mungu, si kipawa cha asili hata kama hakuna kipawa cha asili kisichokuwa zawadi kutoka kwa Mungu. Lakini hapa tunaongelea neema maalum. Mtume Paulo ndiye aliyelitumia mara nyingi neno karama katika barua zake. Anatumia neno karama kama ipawa au uwezo.
Kwa mfano, anamwandikia Timotheo akimwambia hivi: "Usiache kuitumia karama ile iliyomo ndani yako, uliyopewa kwa unabii na kwa kuwekewa mikono ya wazee" (Tim 4:14), na anaendelea kumwambia, "Kwa sababu hiyo nakukumbusha,
uichochee karama ya Mungu, iliyo ndani yako kwa kuwekewa mikono yangu" (2Tim 1:6).
Anachosema Mtume Paulo ni kuwa: kuishi kwa kiasi, uwezo wa kuongoza waamini na kuwafundisha maadili ya kimungu, kwa ujumla ni zawadi (karama) ya Mungu mwenyewe. Lakini karama hiyo inapatiwa nguvu ya kimamlaka kwa ajili ya kutimiza wajibu wake kwa kuwekewa mikono na wazee na Paulo.
Vile vile Mtume Paulo anawaambia Wakristo wa Rumi: «Kwa maana ninatamani sana kuwaona, nipate kuwapa karama za rohoni, ili mfanywe imara» (Rum 1:11). Ukiendelea kusoma Waraka huo huo kwa Warumi, utakuta Mtume Paulo anaeleza hivi: «Lakini karama He haikuwa kama Hie kosa; kwa maana ikiwa kwa kukosa kwake yule mmoja wengi walikufa, zaidi sana neema ya Mungu, na kipawa kilicho katika neema yake mwanadamu mmoja Yesu Kristo kimezidi kwa ajili ya wale
Wengi» (Rum 5:15).
Na anaitaja tena katika Rum 5:16b akisema: "bali karama ya neema ilikuja kwa ajili ya makosa mengi, ikaleta kuhesabiwa haki"
Kumbe basi Karama ni zawadi kutoka kwa Mungu kwa kanisa kwa ajili ya ulimwengu. Karama ya kila familia ya kitawa ni njia maalum ambayo wanashirika wake wanaitwa kumfuata Kristo kwa mfumo huo wa maisha.
Wakarmeli wamejaliwa zawadi -neema -karama ya kuishi maisha ya taamuli/tafakari, maisha ya undugu na maisha ya huduma.
Maisha ya tafakari -Taamuli na sala (Contemplative life)
Tafakari na sala ni moyo wa maisha katika karmeli. Familia ya wakarmeli inaamini kwamba moyo wa njia yetu ya maisha - Hii ni kwa wakarmeli wote, Mapadre, Friars, Masista wa maisha ya ndani au wa maisha ya kitume Utawa wa Tatu, walei, au hermits - moyo wetu wa maisha ni tafakari. Mt. Yohane wa Msalaba aliwahi kueleza kwamba kutafakari ni neema ya Mungu inayotiririka katika mwanadamu. Ni kuwa na urafiki na Mungu kama alivyowahi kusema Padre Joseph Chalmers, O.Carm.
Tokea
siku za kwanza za uwepo wake, jumuiya ya wakarmeli ilifuata mtindo wa
maisha ya taamuli. Mfumo huu umo katika muundo wake na katika thamani
yake au katika tunu zake. Jambo hili linaonekana wazi katika Kanuni
yake ambayo inaeleza kuwa jumuiya ya wakarmeli kama jumuiya ambayo
imejielekeza moja kwa moja katika sala na kuwa makini kwa Neno,
ikimwadhimisha na kumsifu Bwana kwa juhudi zote .
Neno
tafakari au taamuli linaweza kuelezeka kwa ufasaha kuwa ni kutazama na
kuona kwa macho ya kiroho uhalisia wa kimungu, kama asemavyo mzaburi:
«Bali mimi nikutazame uso wako katika haki, niamkapo nishibishwe kwa
sura yako» (Zab 17:15). Ni ile hali ya kutambua uwepo wa Mungu katika
maisha.
Hivyo
kuishi maisha ya tafakari ni kuishi katika uwepo wa Mungu na kuwa naye
ana kwa ana. Msingi wa tafakari ni Neno la Mungu ambalo humtakasa
anayelisoma na kuliishi kwa kuwa ndilo Kweli: «Uwatakase kwa ile kweli;
neno lako ndiyo kweli» (Yoh 17:17).
Lakini
Neno hasa ni Kristo mwenyewe kama tunavyosoma kuwa:«Hapo mwanzo
kulikuwako Neno naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu»
(Yoh 1:1), «Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona
utukufu wake, utukufu kama wa Mwana wa pekee atokaye kwa Baba; amejaa
neema na kweli» (Yoh 1:14). Kumtafakari Neno Aliye Hai ni kuutafakari
utukufu wa Yesu Kristo ambaye hututakasa ili maisha yetu yaweze kufanana
na ya kwake.
Hivyo
maisha ya tafakari katika Karmeli ni kile kipawa anachojaliwa mtu na
Roho Mtakatifu cha kutafuta kuishi maisha ya muungano na Mungu[1].
Japokuwa karama zote tatu haziwezi kutenganishwa, bado kwa namna fulani
msisitizo unawekwa kwenye karama ya maisha ya tafakari kwani ndicho
kiini hasa cha karama nyingine mbili.
Tangu
mwanzoni kabisa mwa ukarmeli, wazee wetu waliishi hii karama pale mlima
Karmeli kwa kuyaelekeza maisha yao yote katika kulisoma na kulitafakari
Neno la Mungu na kuliishi.
Uzoefu
wa namna hiyo unaoneshwa na Samweli. Mwandishi wa kitabu cha kwanza cha
Samweli anasema kuwa, tangu Samweli alipolifahamu Neno la Bwana
alilifanya kuwa sehemu muhimu sana katika maisha yake: “Samweli akakua,
naye Bwana alikuwa pamoja naye, wala hakuliacha neno lake lolote
lianguke chini” (1Sam 3:19). Ndiyo maana hata Mzaburi anasema: “Neno
lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu” (Zab 119:105).
Kwa kuwa karama hii inahitaji ukimya wa ndani, na ukimya wa ndani mara nyingi husaidiwa na utulivu wa nje, basi jumuiya za kikarmeli hutakiwa kuishi katika mazingira tulivu na ya kisala zaidi. Neno la Mungu linapogeuka sala basi ndipo hapo jumuiya nzima husali masifu ya Bwana kwa sauti moja ya kumsifu na kumtukuza.
Mtu
hawezi kumsifu na kumtukuza Mungu kama bado hajaguswa na nguvu za Neno
lake. Ndipo hapo utagundua kuwa karama ya tafakari humwongoza mtu
kuingia katika fumbo la uwepo wa Mungu na hivyo kuutambua ukuu wake na
maajabu anayoyafanya katika maisha ya watu. Neno la Mungu
limewabadilisha watu wengi.
Utakuta
basi kuwa jumuiya za kikarmeli huundwa na watu ambao wanataka
kujiachilia ili waweze kuwa makao ya Roho Mtakatifu ambaye huwabadilisha
kwa vipaji vyake ambavyo ni; usafi wa moyo, mawazo matakatifu, haki,
upendo, imani, na tumaini imara katika wokovu.
Maisha ya tafakari yanamwezesha Mkarmeli kufanya kazi zake katika hali ya amani na utulivu
wa ndani kama Mtume Paulo anavyosema: «Basi twawaagiza hao, na kuwaonya
katika Bwana Yesu Kristo, watende kazi kwa utulivu na kula chakula chao
wenyewe» (2The 3:12).
Tafakari
huanza pale tunapojiaminisha kwa Mungu ambaye hutujia kwa njia yoyote
ile anayoichagua yeye mwenyewe. Kwa namna hiyo, maisha ya tafakari ni
mwelekeo wa ndani au tabia ya kuufungua moyo wote kwa Mungu. Lakini ni
Neno la Mungu ambalo humpatia mwanadamu mwanga ambao huufungua moyo
wake: «Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali
kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili; tena lachoma hata kuzigawanya
nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi
kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo» (Ebr 4:12).
Jambo
hilo hutufanya tutambue uwepo wake mahali popote katika maisha yetu.
Hivyo basi karama ya maisha ya tafakari ni safari ya kiroho na ya ndani
kabisa ya nafsi ya kila mkarmeli anayeungana na Mungu kiroho.
Mungu
ndiye anayemgusa kila Mkarmeli na kumbadilisha kuelekea maisha ya umoja
wa kimapendo pamoja naye. Anamuinua kila aliyetayari kujiachilia ili
aweze kuonja bure furaha kamili ya kupendwa na Mungu na kuishi katika uwepo wake wa kimapendo.
Kwa
jinsi hiyo basi, tafakari ni uzoefu wa nguvu ya Upendo wa Mungu
unaombadilisha kabisa mtu na kumfanya aliye mdhaifu katika kufikiri
mambo matakatifu na kupenda, aweze kufanya hivyo kwa njia ya kimungu
zaidi. Kwa uhalisia wa ubinadamu wetu, kila mmoja anahitaji kuguswa na
Mungu.
Tafakari
au taamuli ina thamani kubwa sana katika maisha ya kila Mkristo. Ndiyo
maana kwa Wakarmeli, tafakari si kwamba ni chemchemi ya maisha ya kiroho
tu, bali pia ndiyo inayoamua na kusaidia ubora wa maisha ya kindugu na
ya utumishi kwa watu wa Mungu. Kwa lugha nyingine, karama ya tafakari
ndiyo inayoziunganisha karama nyingine mbili.
Wakarmeli
popote walipo, wanapofanikiwa kuyaishi kwa uaminifu matunda yatokanayo
na tafakari, pamoja na kuwa katikati ya maisha yenye changamoto za kila
aina, basi huo huwa ndiyo ushuhuda wa fumbo la uwepo hai wa Mungu kati ya watu wake. Mkristo hatakiwi kujenga kisingizio chochote cha kutopata muda wa kukaa na kuongea na Mungu.
Ndiyo
maana kazi ya kuutafuta uso wa Mungu na upokeaji wa zawadi za Roho
Mtakatifu inazifanya jumuiya za Wakarmeli kuwa angalifu zaidi katika
kuzitambua alama za nyakati na wakati huo huo kuwa makini zaidi katika kuzitambua mbegu za Neno wa Mungu.
Hapo
ndipo unapokuja kugundua kuwa maisha ya taamuli au tafakari huzingatia
na hutathmini matukio mbalimbali ya kihistoria yatokeayo ndani ya
Kanisa, duniani na sana sana katika jamii za watu wa kawaida, kwa lengo
la kutoa msaada unaohitaji kulingana na mapenzi ya Mungu.
Kwa
njia hiyo basi Wakarmeli kwa kumfuata Yesu Kristo, huonyesha mshikamano
kwa kuhamasisha matukio yaletayo matumaini na upendo katika jamii. Kwa
kuyatafakari yote yanayotokea katika ulimwengu huu, na kwa kuongozwa na
Neno la Mungu, Wakarmeli hujitahidi kufanya maamuzi ambayo huchangia
kuyabadili maisha ya watu wengi ili maisha na matendo yao yalingane na
mapenzi ya Mungu Baba.
Nirudie
kusisitiza kuwa, ili maisha ya taamuli –tafakari yaweze kuzaa matunda,
hutakiwa ukimya wa kweli wa ndani ambao humpa nafasi Mungu ya kuongea.
Kutokana na kuhitajika kwa ukimya wa ndani hata mazingira ya nje
hutakiwa yawe ya ukimya pia. Ukimya wa nje hurahisisha zoezi la kuzama
ndani kabisa mwa nafsi na kuungana na Mungu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni
Zingatia: Mwanachama wa blogu hii tu ndiye anayeweza kuchapisha maoni.